11:00 Baadhi ya waliowania urais wamefika ukumbini na kuketi. Mmoja wao ni mgombea wa ADC Hamad Rashid.
10:30 Wanahabari, waangalizi na maafisa wengine wa uchaguzi tayari wamo ukumbini wakisubiri kuanza kutangazwa kwa matokeo.
10:20 Kulikuwa na wagombea 14 kwenye karatasi za kura za kumchagua rais. Majina yao ndiyo haya:
1
Khamis Iddi Lila
ACT-W
2
Juma Ali Khatib
ADA-TADEA
3
Hamad Rashid Mohamed
ADC
4
Said Soud Said
AFP
5
Ali Khatib Ali
CCK
6
Ali Mohamed Shein
CCM
7
Mohammed Massoud Rashid
CHAUMMA
8
Seif Sharif Hamad
CUF
9
Taibu Mussa Juma
DM
10
Abdalla Kombo Khamis
DP
11
Kassim Bakar Aly
JAHAZI
12
Seif Ali Iddi
NRA
13
Issa Mohammed Zonga
SAU
14
Hafidh Hassan Suleiman
TLP
10:15 Ulinzi mkali umewekwa katika ukumbi wa kutangazia matokeo. Mbwa wa ulinzi pia wametumika kukagua eneo hilo, ambalo mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar Selim Jecha Selim anatarajiwa kutumia kutangaza matokeo.
10:00 (Saa za Afrika Mashariki). Hujambo! Matokeo ya mapema ya uchaguzi wa marudio uliofanyika visiwani Zanzibar Jumapili yanatarajiwa kutangazwa leo.
Karibu kwa taarifa za moja kwa moja kuhusu kutangazwa kwa matokeo hayo.
Post a Comment