Loading...

HABARI ZA HIVI PUNDE: MOJA KWA MOJA MATOKEO YA UCHAGUZI ZANZIBAR

Bofya hapa kwa habari za karibuni zaidi
11:00 Baadhi ya waliowania urais wamefika ukumbini na kuketi. Mmoja wao ni mgombea wa ADC Hamad Rashid.
10:30 Wanahabari, waangalizi na maafisa wengine wa uchaguzi tayari wamo ukumbini wakisubiri kuanza kutangazwa kwa matokeo.
10:20 Kulikuwa na wagombea 14 kwenye karatasi za kura za kumchagua rais. Majina yao ndiyo haya:
1Khamis Iddi LilaACT-W
2Juma Ali KhatibADA-TADEA
3Hamad Rashid MohamedADC
4Said Soud SaidAFP
5Ali Khatib AliCCK
6Ali Mohamed SheinCCM
7Mohammed Massoud RashidCHAUMMA
8Seif Sharif HamadCUF
9Taibu Mussa JumaDM
10Abdalla Kombo KhamisDP
11Kassim Bakar AlyJAHAZI
12Seif Ali IddiNRA
13Issa Mohammed ZongaSAU
14Hafidh Hassan SuleimanTLP
10:15 Ulinzi mkali umewekwa katika ukumbi wa kutangazia matokeo. Mbwa wa ulinzi pia wametumika kukagua eneo hilo, ambalo mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar Selim Jecha Selim anatarajiwa kutumia kutangaza matokeo.
10:00 (Saa za Afrika Mashariki). Hujambo! Matokeo ya mapema ya uchaguzi wa marudio uliofanyika visiwani Zanzibar Jumapili yanatarajiwa kutangazwa leo.
Karibu kwa taarifa za moja kwa moja kuhusu kutangazwa kwa matokeo hayo.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright NEWZ | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top