Loading...

Wagombea warushiana matusi Marekani

Image copyrightAP
Image captionWagombea wa urais nchini Marekani kupitia tiketi ya chama cha Republican Ted Crus na Donald Trump walirushiana cheche za matusi katika mjadala
Wagombeaji wawili wa Urais wa chama cha Republican nchini Marekani wamegombana vikali na kurushiana matusi juu ya wake zao.
Seneta wa Texas, Ted Cruz, amemlaumu mpinzani wake, mfanyabiashara Donald Trump kwa kuzusha uvumi kuwa yeye alikuwa mzinifu na kumdanganya mkewe, Heidi.
Bwana Cruz alisema uvumi huo ni takataka na akasema kuwa anaelewa kuwa uvumi ulianzishwa na Bwana Trump ambaye alisema hastahili kuwa Rais.
Bwana Trump alisisitza kuwa hakuhusika vyo vyote na uvumi huo.
Image copyrightGetty
Image captionMjadala wa wagombea urais nchini Marekani
Mapema juma hili, Bwana Trump alimlaumu Seneta Cruz kwa kuweka picha za mkewe, Melania, akiwa uchi kwenye mtandao ili kumharibia sifa.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright NEWZ | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top