Loading...

UKAWA WAKINUSHA TENA BUNGENI, KIONGOZI WA KAMBI YA UPINZANI FREEMAN MBOWE AGOMA KUWASILISHA HOJA NA KUFUNGUKA MAZITO

Pg 1c
Watoa hoja tatu mwiba kwa Serikali ya JPM, dalili za kususia bajeti waziwazi
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
KIONGOZI wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, jana aligoma kuwasilisha maoni ya kambi hiyo akitoa hoja tatu zilizosababisha kuchukua uamuzi huo ambazo pia zinaweza kuwa chanzo cha wao kususia bajeti.
Hoja hizo ni Serikali ya Rais Dk. John Magufuli kufanya kazi bila ya kuwa na mwogozo wowote wenye msingi halali wa kisheria katika wizara zake, uvunjaji wa Katiba na sheria za nchi kuhusiana na Bajeti na Serikali kupoka madaraka na uhuru wa mhimili wa Bunge.
Katika hilo, Mbowe alilieleza Bunge kuwa Kambi ya Upinzani Bungeni haitakuwa tayari kuendelea kushiriki uvunjaji wa Katiba, Sheria na haki za msingi za wananchi na kwamba wanatafakari kwa kina na makini hatua za kufuata.
SERIKALI KUTOKUWA NA MWONGOZO
Mbowe ambaye alikuwa akiwasilisha taarifa ya Kambi ya Upinzani wakati wa kipindi cha jioni, alisema kutokana na kukosekana kwa mwongozo halali wa kisheria katika wizara za Serikali ya Rais Magufuli, inaonyesha kiongozi huyo hajaiunda kihalali Serikali yake.
Akifafanua hilo Mbowe alisema kiongozi huyo wa nchi ameshindwa kutekeleza sheria ya utekelezaji wa majukumu ya mawaziri ya mwaka 1980, ambayo inaweka masharti ya kutengeneza mwongozo wa muundo na utekelezaji wa majukumu ya Serikali yake.
Alisema sheria hiyo pamoja na mambo mengine kila linapotaka kuundwa Baraza la Mawaziri inamtaka rais kuchapisha katika gazeti la Serikali kueleza jinsi Serikali yake itakavyotekeleza majukumu yake, jambo ambalo halijafanyika na badala yake Serikali imekuwa ikifanya kazi kwa kauli za rais na mawaziri bila kufuata mwongozo wowote.
“Sheria ya Utekelezaji wa majukumu ya mawaziri ya mwaka 1980, kifungu cha 5(1) kinaweka masharti kwa rais kutengeneza mwongozo wa muundo na utekelezaji wa majukumu ya Serikali yake.
“Mpaka sasa mwongozo wa utendaji wa Serikali kwa kila wizara (Instrument) unaotumika ni ule uliochapishwa kwenye gazeti la Serikali namba 494A la tarehe 17/12/2010. Kwa mujibu wa Instrument hiyo, majukumu ya Ofisi ya Waziri Mkuu ni Coordination of Government Business, Leader of Government Business in the National Assembly, Link between Political Parties and Government, National Festivals and Celebration of Management of Civic Contingencies (relief).
“Mheshimiwa Spika, kitendo cha Serikali hii kuendesha kazi zake kwa mwongozo wa 2010, ina maanisha kwamba majukumu ya Ofisi ya Waziri Mkuu bado ni yale yale yaliyochapishwa mwaka 2010, kwa sababu gazeti hilo la Serikali halijafutwa,” alisema Mbowe huku akishangiliwa na wabunge wa upinzani.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright NEWZ | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top