Loading...

Apigwa Risasi na Kuuwawa na Majambazi Mbezi

Jana usiku yametokea mauwaji ya mtu mmoja mwanaume kwa kupigwa risasi na watu wanaosadikiwa kuwa majambazi katika Bar ya Kadabla iliyopo katikati ya Mbezi kwa Msuguli na Kibanda cha Mkaa.Mauwaji hayo yametokea kati ya majira ya saa tano usiku hadi saa saba usiku

Mashuhuda wa tukio katika eneo hilo wanasema marehemu alifika katika Bar hiyo ambayo amezoea kufika mara kwa mara anapokuwa anatoka kwenye mihangaiko yake maeneo ya K'koo,usiku wa jana alifika akiwa peke yake na kuegesha gari kisha kuanza kupoza koo.

Baada ya muda kupita,alimpigia mkewe ambaye wanaishi nae maeneo ya Mbezi Mwisho eneo la Tanesco njia ya kwenda Malamba Mawili,wito huo kwa mkewe ilikuwa kwa ajili ya kukaa wote ili waagize "kitimoto" na kuburudika pamoja.Katika ya burudani ya moja moto na mbili baridi huku kitimoto ikiwa inakaangwa jikoni kwa Mangi,walikuja watu wasiopungua wawili na kuanza kugongagonga gari lake,ilibidi aamke ili kujua kulikoni watu hao kugonga gari lake?

Baada ya maulizo hayo,wale jamaa wakamwambia wao wanataka pesa,wanajuwa ana pesa ndani ya gari,hivyo wanazitaka.Yakatokea mabishano na baadae jamaa wakampiga risasi mbele ya mke wake na kuchukua maisha yake huku wakitokomea na kiasi cha pesa kilichokuwepo.Kulizuka taharuki na watu kuacha vinywaji vyao na chakula juu ya meza na kutawanyika,hata waliokuwa "tungi" waliweza kukimbia bila kuyumba.

Msiba uko nyumbani kwa marehemu maeneo ya Mbezi Mwisho(Tanesco Maghorofani) njia ya kwenda Malamba Mawili.Bwana alitoa na bwana ametwaa,Jina lake lihimidiwe.

Polisi iamke na kutazama matukio haya ya uhalifu maana watu wanauwa wazi wazi na silaha za moto zimeenea hovyo hovyo.

Wimbo wa Aje Ilikuwa Suprise kwa Wema Sepetu – Alikiba Afunguka


Akiongea kwenye kipindi cha Friday Night Live, Alikiba almesema wimbo huo hajamuimbia Jokate na wala hajawahi kumuimbia mtu yeyote, bali aliimba kwa ajili ya mashabiki wake.


” Sijamuimbia mtu yeyote kwa kweli, mi nimeimba kwa ajili ya mashabiki wangu, kwanza sijawahi kumuimbia mtu kabisa, sijawahi, so ni kwa ajili ya mashabiki wangu”,.

Lakini pia Alikiba alisema kuwa kitendo cha kuwataja wasanii wa Filamu Wema Sepetu na Lulu kwenye wimbo huo, ilikuwa ni suprise, hivyo wenyewe hawakujua kuwa wameimbwa, isipokuwa alishawahi kumdokeza Wema Sepetu ambaye ametaja kuwa ni rafiki yake mkubwa.

“Wenyewe walikuwa hawajui kuwa nimewaimba, ila Wema nilimwambia siku moja kuwa bichwa nina suprise yako, ila Lulu sikuwahi kumwambia na hata sijui ameipokeaje, ila naamini kaipokea fresh”, alisema Alikiba.

Kitu ambacho bado kinawapa kigugumizi watu ambao walikuwa wakifuatilia kipindi hicho, pale aliposhindwa kuchagua kati ya Wema Sepetu na Jokate, na kusema anawachagua wote, na kuzidi kuweka hali ya sintofahamu kwa wawili hawa (KIba na Jokate) huenda bado wako pamoja.

BREAKING NEWS NI ZAIDI YA AIBU NI LAANA CHAFU ALIOYOFANYA MSHAURI WA RAIS SHEIN KUTWA AKILA ARODA BINTI MDOGO WA MIAKA 20 HILI NI TUKIO LA PILI TENA ZANZIBAR....

Dk. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar (katikati) akipokea ripoti kutoka kwa Dadi Faki Dadi aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba.
SERIKALI ya Dk. Ali Mohammed Shein imezama kwenye aibu, ni baada ya mshauri wake Dadi Faki Dadi kukamatwa kwa tuhuma za kufanya ngono na mwanaye, anaandika Pendo Omary.
Faki alikuwa Mkuu Mkoa wa Kaskazini Pemba lakini baada ya kukosa nafasi hiyo katika ngwe ya pili ya Dk. Shein, aliteuliwa kushika nafasi hiyo ya ushahuri kwa rais hususan masuala ya yanayohusu Pemba.
Mshauri huyo amekamatwa kwa tuhuma za kufanya ngono na mtoto wake wa kambo (mtoto wa mkewe) mwenye umri wa miaka 21.
Mwanasiasa huyo maarufu visiwani humo alikamatwa mbele ya mkewe na baadhi ya wanafamilia juzi katika nyumba ya wageni ya Executive, jirani na Makao Makuu ya Uhamiaji Zanzibar, eneo la Kilimani mjini Unguja na kupelekwa katika kituo cha Polisi Mwembemadema.
Mkadam Khamis, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi amethibitisha kushikiliwa kwa Dadi na polisi kwa muda kabla ya kumwachia kwa dhamana wakati uchunguzi wa tukio hilo ukiendelea.
“Tunaendelea kufanya uchunguzi. Iwapo tutabaini ametenda kosa tutampeleka katika vyombo vya sheria,” amesema Khamis.
Aidha, picha za video ambazo zinaendelea kusambazwa katika mitandao ya kijamii zinamuonesha Dadi akishambuliwa kwa maneno makali kutoka kwa mkewe na watu waliomkamata.

Mambo ya Msingi Kuyafanya Kabla ya Kuoa/Kuolewa

Ndoa nyingi zinaingia kwenye migogoro kwa sababu ya mambo ya kukurupuka na kufanya haraka bila wahusika kufahamiana vizuri, hebu tuzingatie yafuatayo ili tusiseme 'NINGEJUA NISINGEOA/NISINGEOLEWA'

1. Chanzo cha uhusiano wenu kiwe ni upendo wa dhati
2. Chunguza kwa mwenzio juu ya tabia:nidhamu, adabu, hasira, ulevi na umalaya
3. Mpeane muda wa kutosha kufahamiana
4. Mtembee pamoja maeneo tofautitofauti kama michezoni, bar na out mbalimbali ili muone interest za kila mmoja
5. Muwe wa imani moja. ila kama mmeshibana sana na mwaweza kuvumiliana hata wa imani tofauti ni sawa.
6. Wajue ndugu wa mwenzio ili kupata habari zao zitakazokufahamisha mwenzao pia yukoje
7. Pimeni afya zenu bila aibu. kuna maradhi mengi kama HIV/AIDS na mengine.
8. Kama ni Mkristo au Muislam funga ndoa Kanisani au Msikitini na siyo Bomani.
9.Kwa Wakristo ndoa haina talaka. huu ni mpango wa Mungu. kuachana na kuoa mwingine ni dhambi.

N.B: kama mwenzio ana tabia usiyoipenda, usifunge ndoa naye ukitegemea atabadilika.abadilike wakati mkiwa wachumba na siyo kwenye ndoa, labda kama umeshamkubali kama alivyo

HABARI YA HIWVI PUNDE: MTOTO WA MIAKA MINNE ATOA SIRI NZITO NA MKASA WOTE WA TUKIO LA MAUWAJI YA ANETH MSUYA MSIKILIZE HAPA MTOTO HUYU HUU NI ZAIDI YA UNYAMA ALIOFANYIWA DADA HUYU....


             
May 26 kulitokea mauaji ya kutisha ya kukatwa mapanga kwa mwanadada Aneth ambaye ni ndugu wa Tajiri mmoja ambaye naye aliuliwa kwa kupigwa risasi. Aneth amepigwa mapaga na watu wasiojulika na kukimbia. Jirani wa Anetha pia mfanyakazi mwenzake anafafanua vizuri,
     “Yaani Aneth hata siamini, jana tulikua nae kazini, kaondoka kufika nyumbani akakuta housgal katoroka, akapiga simu kwa mwenzetu akamueleza kwamba leo hatokuja ili angalie logistics. 
 Mtoto wake ana miaka minne ndio alipo hojiwa alisema hivi jana walikuja watu watano weusi, wakavunja mlango ni majira ya mama saa tatu usiku, akakimbia chumbani, walipoingia wakamkuta mtoto wakauliza mama huko wapi akasema chumbani, wakamfuata huko mtoto hajui kilichoendelea. hadi  asubuhi school bus ilipokuja alijaribu kutoka akashindwa na mwishowe iliondoka.
Anafafanua: Baada ya kuona mama yake haamki ndipo alipotoka kwa jirani na kuwaita. Majirani walikwenda na kukuta Aneth akiwa amechinjwa na akiwa uchi (seems walimbaka) kisu kipo hapohapo na hawajaiba kitu.

Inasemekana alikuwa anafyatilia sana kes ya marehem kaka ake Msuya yule bilionea wa arusha aliuawa kwa kupigwa risasi

BREAKING NEWS: RAIS MAGUFULI SASA HASHIKIKI TENA HII MOJA YA TUKIO LA KIHISTORIA KATIKA UTAWALA WAKE MPAKA SASA AMUA WAZIWAZI KUPINGANA NA UKWELI WA JAMBO HILI NA KUAMUA HAYA....

anayepingana na ukweli kwamba ‘Wazee ni hazina ya Taifa la Tanzania’ lakini acha  ukweli uzungumzwe, kwani ‘kubebana’ na‘kuleana’ kumetufikisha hapa tulipo.

Tabia iliyojengwa na wazee ya kufanya kazi kwa mazoea huku waking’ang’ania madaraka kunalifanya taifa kupiga ‘mark time’ badala ya kusonga mbele; tafiti zinaonesha asilimia kubwa ya vijana wasomi wapo mitaani na hawana ajira kutokana na nafasi hizo kukaliwa na wazee, tena ambao hawana elimu sawa na vijana wasomi ambao wanasota mitaani.

magufuliJambo hili linamfanya Rais wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli kuamua kufanya kazi na vijana katika serikali yake kwani amegundua licha ya vijana wachapakazi kutopendwa na baadhi ya watu, ni wachapakazi na watamsaidia kulipeleka taifa katika maendeleo anayoyatamani, kutokana na ukweli kwamba wengi wao hawapendi rushwa.

“Nimegundua vijana wengi hawapendi rushwa, hivyo nitaongeza vijana kila nikiteua kwa kuwa niliowaweka naona matunda ya kazi zao, najua watu wanawachukia sana ila nitawaongeza. Palipo na vijana nimeona mambo yanaenda na kuna mabadiliko. Wazee ndio tumelifikisha taifa hili hapa, hakuna asiyejua kuwa Tanzania ilichakaa kila mahala”.

mbarawaNi wazi hivi sasa wazee wamekalia kuti kavu katika Serikali ya Awamu ya Tano kwani Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa amefuata nyayo za Rais Magufuli katika ‘operesheni fukuza wazee’ baada ya kutamka wazi kwamba wakati umefika kwa wazee wanaofanya kazi katika Kampuni ya Simu ya TTCL kuwaachia Vijana kwa sababu wazee wamekua watu wa kuzungumza zaidi kuliko vitendo kwani Sekta ya Mawasiliano hivi sasa ina ushindani mkubwa.

Isabela Afunguka 'Inaniuma Sana Kalama Kuniacha Mimi na Kumuoa Shoga Yangu'

Luteni Kalama na Mkewe aliyefunga naye ndoa hivi karibuni

SIKU chache baada ya Mbongo Fleva, Kalama Bakari ‘Luteni Kalama’ kuvuta jiko, hatimaye, aliyekuwa mchumba wa muda mrefu wa msanii huyo ameibuka na kusema anaumia kuona aliyeolewa alikuwa ni rafiki yake wa karibu.

Kalama alimuoa binti aitwaye Aisha Yassin wiki iliyopita ambapo saa chache baada ya ndoa hiyo kufungwa na picha kusambaa mitandaoni, wapenda ubuyu waliibuka na kuanza kueleza kuwa Kalama ameona shosti wa Isabela.

“Hili jambo sio siri limetuacha midomo wazi sisi tunaowajua vizuri hawa watu, walikuwa wanajifanya shemeji shemeji huku wanazima taa, isitoshe kwanza nasikia ana mtoto wa mwaka mmoja, yani ni majanga tupu, bora angemuachia Isabela aendelee na mtu wake waliyetoka mbali,” alisema mdaku mmoja.

Akiizungumzia ishu hiyo, Isabela alisema ameumia kuona Kalama amekwenda kwa rafiki yake kwani bora angemchukua mtu mwingine.
Luteni Kalama akiwa na Mkewe wa zamani, Isabela Mpanda

“Nimeumia. Rafiki yangu wa damu ambaye alikuwa anakuja tunakunywa wote na akionyesha kumheshimu Kalama kama shemeji yake eti leo kanigeuka, hii yote sababu yule mwanaume naye anapenda kulelewa halafu yule demu kidogo yupo vizuri kifedha.

“Japo nilikuwa nimeshamuacha Kalama kwa kuwa niliona ananipotezea muda, niliumia sana kwamba kwa nini awe rafiki yangu? Mungu atawaadhibu,” alisema Isabela.

Alipotafutwa Kalama na kusomewa mashtaka ya Isabela, alisema mwandani wake huyo wa zamani kakosa cha kuongea yeye aliachana naye kwa kuwa walishindwana na wala huyo mke wake hakuwa rafiki yake.

“Anatapatapa tu Isabela, ninachofahamu mimi ndio mume halali wa Aisha, kuhusu kuwa rafiki yake wala Bela hamjui huyo mwanamke vizuri, sioni cha ajabu kuoa mtu mwenye mtoto, atuache tufurahie maisha ya ndoa,” alisema Kalama.

John Heche: Rais wa China Alipokuja Tanzania Aliondoka na Pembe za Tembo

Akichangia kwenye bajeti ya mali asili na utalii mbunge John Heche amezungumzia operesheni tokomeza jinsi ilivochezea watu rafu na kuuawa kama wanyama.

Hapo hapo amegusia kuwa Rais wa China alipokuja Tanzania aliondoka na pembe za tembo na hii iliripotiwa na vyombo vikubwa vya habari duniani kama Al Jazeera na BBC lakini serikali haikujibu wala kuchukua hatu.

Lakini serikali hii iliwaua wananchi na kuua mifugo yao ili kutokomeza ujangiri kumbe majangiri ndio wao wenyewe 

Video : Idriss Alimfanyia Wema Sepetu Haya, Mara Baada ya Kusikia Wema Sepetu Katukanwa na Harmonize

Baada ya kusambaa kwa video ya Harmonize akimsema vibaya Wema Sepetu, watu wengi walilaani kitendo hicho huku kuna baadhi yao wakimpongeza Harmonize. Habari kutoka kwa marafiki wa karibu wa Wema Sepetu zinasema kua aliumia sana alipoiona video hiyo kwa mara ya kwanza.

Wengi walitaka kujua Idriss alipokeaje swala hilo, basi hii ni Exclusive kutoka kwa Wema akielezea kitu alichofanyiwa na Idriss na kumtia moyo katika kipindi hicho kigumu. Wema alimshukuru sana Idriss kwa wema wake,

Unaweza tazama video ya alichokisema Wema Hapa....

Video : Sikiliza Kionjo cha Wimbo Mpya wa Nay Wamitego - Kati Patamu...TCRA Watauacha??

Wengi wanamjua Nay Wa Mitego kwa kutoa nyimbo nyingi sana zikiwa za utata, mara nyingi hua anawachana watu maarufu bila kuwaogopa au ujumbe ndani ya nyimbo kua na utata. Haya basi katika pitapita zetu tumepata kionjo cha wimbo wake mpya ambao bado haijajulikana hasa utatoka lini.

Wimbo huo unaenda kwa jina la pale kati patamu, kwa tafsiri za kwetu mtaani nina uhakika kabisa kua huu wimbo ukiachiwa utakua gumzo sana . Sio tu mtaani hata huko mitandaoni ambapo nadhani TCRA wanaweza kufanya yao. Unaweza skiliza video ya wimbo huo hapa chini......

Older Posts
© Copyright NEWZ | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top