Loading...

Rais Magufuli na Mkewe Waguswa na Stori ya Mwanafunzi wa Chuo Kikuu Aliyepofuka Macho..Waamua Kumchangia Mil 10 Akatibiwe



Baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DktJohn Pombe Magufuli, Mkewe Mama Janeth Magufuli na familia yake kuahidi kuchangia Milioni 10 kwaajili ya matibabu ya #Kipepeo Bernadeta Msigwa mwakilishi kutoka ofisi ya Rais Bw. Ngusa Samike amefika katika ofisi za CloudsMediaGroup na kukabidhi fedha hizo. Vilevile Mheshimiwa Rais ametoa ujumbe kwa Kipepeo Bernadeta kuwa amtumainie Mungu kwani ndiye muweza wa kila kitu. Katika upande mwingine Naibu wa Waziri wa Wizara ya Kazi, Vijana na Ajira Mh. Anthony Mavunde amechangia Shilingi Milioni 1.
Kama umeguswa na unahitaji kuchangia au unataka maelezo zaidi kuhusu jinsi ya kumsaidia piga namba 0742848729. Pia unaweza kuangalia story yake kamili kwenye account hii ya Instagram@BernadetaMsigwa.
Asante sana Mh. Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright NEWZ | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top